-Marcus Rashford amesema anataka aongezewe mshahara ili aweze kusalia katika klabu ya Manchester United
– Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 21 amesalia na miezi 12 pekee kuchezea klabu hiyo hiyo kulingana na mkataba wake
-Aidha, inakisiwa kuwa anamezewa mate na klabu ya Barcelona na huenda akanunuliwa wakati wowote
– Meneja wa klabu hiyo Ole Gunnar Solskjaer yuko macho asinyakuliwe na mabingwa wa La Liga
Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United, Marcus Rashford ameripotiwa kuitisha mshahara wa pauni 300,000 kila wiki kutoka kwa klabu hiyo la sivyo agure uga wa Old Trafford.
Rashord, ambaye amesalia na miezi 12 kuchezea klabu ya Man U kulingana na mkataba wake, ametishia kujiunga na wenzake Paul Pogba na David de Gea.
Habari Nyingine: Kiungo wa Harambee Stars Ayub Timbe ajitolea kuwanunulia mashabiki tikiti za Afcon
Habari Nyingine: Chelsea: Maurizio Sarri ajiunga rasmi na Juventus
Tishio la kiungo huyo wa mbele lamuacha meneja wa kikosi hicho kuingiwa na tumbo joto kwa hofu kuwa huenda akajiunga na miamba hao wa Uhispania kwa uhamisho wa bure.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21, anamezewa mate na klabu ya Barcelona na huenda akajiunga nao iwapo viongozi wa Manchester United watashindwa kutimiza matakwa yake.
Kwa sasa Rashford anapania kutia mfukoni pauni 300,000 kila wiki kama Alexis Sanchez japo ya kutokuwa na uzoefu wa kutosha katika kusakata dimba.
Hata hivyo, kulingana na ripoti ya ‘The Mirror’, Rashford, anadai kutokuwa na haraka ya kugura klabu yake ya utotoni licha ya kuwataka wakuu wa klabu hiyo kumsikiza.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected]; [email protected] au WhatsApp: 0732482690. Tufuate kwa Telegram: Tuko news.
Source: Tuko